Hivi karibuni kumekuwa na viongozi wengi
wa Dini wanaowania nafasi za kisiasa. Wanasiasa wanawasakama
kuwa wanachanganya DINI na SIASA. Siasa na DINI zitenganishwe?
Kweli serikali haina dini? Nini maoni yako kuhusu hilo?
Wewe
Unasemaje?

Siasa na DINI Hazichanganyiki
- Munishi
Dini
na siasa ni mafuta na maji. Haziwezi kuchanganywa hata kidogo.
Zitenganishwe. Maneno kwamba serikali haina dini ni kufuru
kwa Mungu.Huwezi kuwakuta watu na dini zao, halafu uwape kadi
za CCM uwaite wanachama wa CCM wasiyo na dini. Huo ni wendawazimu.
Mbaya zaidi CCM wakitumia kila mbinu chafu kushinda uchaguzi
wanaunda serikali ya mabavu na wanatangaza hadharani kuwa
chama na serikali havina dini. Hiyo
siyo kweli.
Waumini
wa dini wanadanganywa na wanasiasa hapa. Lazima tujue kuwa
wakati wa kutengana na wanasiasa umefika. Kila muumini wa
dini yeyote tangu leo asiwe mwanachama wa chama chochote cha
kisiasa. Tuwaache wanasiasa watafute wanachama wasio na dini
ili wawaandikishe katika vyama vyao. Wakisema chama chao hakina
dini watakuwa wakisema ukweli. Pia wakiunda serikali yao waseme
chama na serikali havina dini watakuwa wanasema ukweli mtupu.
Wewe
Unasemaje?

Pope
aafiki dini itenganishwe na siasa.
Ni
rahisi sana kutenganisha Dini na Siasa iwapo tu wale waliona
majukumu ya kufanya hivyo wataamua kufanya hivyo, ni hatari
sana kuvipeleka vitu hivi sambamba kwa kuwa waumini huwa ni
watiifu sana kwa kiongozi wao wa Dini. Hivyo basi ni rahisi
kwao kufuata kiongozi wao mathalani kama nimpenzi au mfuasi
wa chama fulani, mfano mzuri ni kwa Chama cha CUF wamekihusisha
mnoo na Uislamu na matokeo yake tumeyaona Serikali ikipingana
na CUF basi inapingana na Uislamu kwa Ujumla ingawa sio waislamu
wote lakini wengi wao na hasa Zanzibar .
Sehemu
zote za mwambao wanaamini hivyo, hivyo naonelea ni bora Dini
na Siasa vitenganishwe hasa kwa hawa viongozi wadini au wa
Jamii husika kama mtu Padri awe padri tuu na kama mtu ni mwenyekiti
wa Chama Fulani ni bora awe hivyo tu, Pili: Si dhani kama
Serikali ina Dini maana ninavyoelewa mie ni kuwa kama serikali
ingekuwa ina Dini basi ni wazi kungekuwa na Sheria mama za
Dini ile mfano Afghanstan au Vatican na Nchi nyingine nyingi
za Kiarabu imbazo zinaongozwa chini ya Dini ya Kiislamu, Hivyo
sidhai kama serikali yetu ina dini.
Wewe
Unasemaje?

Munishi
afafanua zaidi
POPE tuko pamoja
kwa hilo. Mimi naongezea tu.
Dini na siasa siyo kwamba haziwezi kuchanganywa, bali moja
iko kimakosa duniani. Siasa haiwezi bila dini, lakini dini
inaweza pasipo siasa, kwa hiyo tunataka dunia isiyo na kitu
kinachoitwa siasa.
Dini ni itikadi au imani inayomhusu mwanadamu na Mungu, wakati
siasa ni itikadi au imani inayomhusu mwanadamu na mwanadamu.
Siasa ni mwanadamu kumdanganya mwanadamu mwenzake kuwa anaweza
kumsaidia mambo yote yanayomhusu hapa duniani bila Mungu,
wakati dini inaweza kwa hakika kumsaidia mwanadamuhapa duniani
na baadaye inamhakikishia uzima wa milele mbinguni.
Kwamba wanasiasa wanataka waachiwe siasa, na wahubiri wanataka
kuingia siasa , hawa wote wawili wamechanganyikiwa. Ukweli
ni kwamba lazima moja kati ya siasa na dini ikome kufanya
shughuli zake kwa wanadamu.
Na kwa sababu dini inaweza kumsaidia mwanadamu kiroho na kimwili,
basi lazima siasa isimamishe mara moja shughuli zake duniani
kote. Yenyewe ndio inayojaribu kuyachukua majukumu ya Mungu
kumwongoza na kumsaidia mwanadamu wakati inajua fika kuwa
haiwezi.
Ukiwasikia wanasiasa wakiwaambia viongozi wa kidini waachane
na siasa, waambieni kuwa wao ndio wanaotakiwa kuachana na
siasa ili wajiunge na dini, maana dini ni mambo yote. Ya hapa
duniani na ya huko mbinguni. Hakuna kiongozi wa kidini atakayethubutu
kuiacha dini ajiunge na wanasiasa waongo na matapeli. Nawaita
matapeli kwa sababu wanaitawala dunia kinyume na mwenye dunia
alivyopanga itawaliwe. Mungu alipanga dunia itawaliwe na watumishi
wake aliowaita na siyo wanasiasa waliojiweka madarakani kwa
njia zisizo halali. Waulize viongozi duniani kote swali hili:
Nani aliwatawaza kuwa viongozi? na utashangaa kusikia majibu
yao.
Wengine watasema walichaguliwa na watu katika uchaguzi ulio
kuwa huru na haki, kumbe rushwa ndio iliutawala uchaguzi.
Afrika tuna viongozi waliochaguliwa katika mazingira ya ajabu
sana.
Wananchi wanaaza kudanganywa na vyombo vya habari kwani karibu
wote wanaosikika au kuonekana kwenye vyombo hivyo wakati wa
uchaguzi mkuu lazima wawe walitoa rushwa.
Cha ajabu ni kwamba baada ya uchaguzi vyombo hivyo hivyo ndio
vinakuwa mstari wa mbele kulaani rushwa ndani ya viongozi
wale wale walioingia uongozini kirushwa. Ikiwa wao walipokea
wakati ule, basi wana haki gani kuwakataza viongozi wasipokee
ili kurudisha pesa zao. Jamii imetumbukizwa katika dimbwi
la rushwa na wale ambao walitakiwa wawe wa kwanza kuipiga
vita.
Ni mpaka utaratibu unaotumika kuwachagua viongozi ubadilishwe,
ndipo tunapoweza kusema kuwa tuna jamii ambayo haina rushwa.
Tumuache Mungu atuchagulie viongozi ambao wataongoza kwa kuzingatia
yale Mungu anayoyataka. Pia wale viongozi walioko wakitubu
na kuisikiliza sauti ya Mungu na kuitii, basi nchi zao zitakuwa
na baraka tele.
Mungu anasema kuwa wanasiasa waachane na siasa na wajiunge
na Injili ya kweli ya Yesu mwokozi. Watubu dhambi zao zote
na Yesu atawasamehe na kuwapa uwezo wa kufanyika wana wa Mungu.
Baada ya hayo wangoje kuisikia sauti yake Mungu ikiwaita katika
uongozi.
Wewe
Unasemaje?

Erikisen
asema zitenganishwe!
Ni
kweli serikali yetu haina dini. Na sidhani kama ni busara
kwa serikali ya Tanzania kuwa na dini kwa sababu ya mchanganyiko
na uwiano wa dini nyingi zilizopo. Tutawasha moto. Kutenganisha
dini na siasa pia ni muhimu. Zama za waisraeli wa biblia siasa
na dini ilikuwa kitu kimoja, sio leo.
Wewe
Unasemaje?

Huwezi
kutenganisha Siasa na Dini: Kimeta Jr
Watu
wamekuwa wakiimba wimbo huu wa kwamba dini na siasa vitenganishwe
tangu siku nyingi. lakini mimi naona wengi wanaodai hivyo
hawaelewi. Kwa upande wangu na mtazamo wa wanazuoni huwezi
kutenganisha dini na siasa.
Dini
na siasa ni vitu vinayaendesha maisha ya kila binadamu.Kwa
upande mwingine dini imekuwa chanzo kizuri cha kujenga msingi
imara wa kisiasa kwa mataifa mengi.Tukumbuke kuwa kiongozi
na raia mzuri kwa nchi yake ni yule mwenye dini na anaye mjua
na kumwogopa Mungu au Allah, kwa kuwa kama atamwogopa Mungu
kwa sababu ya dini yake, awe mpagani, mkristo au mwislamu,
ataiheshimu kazi ya uumbaji Mungu aliyoifanya kwa siku saba.
Hivyo suala la kutenga dini na siasa halina msingi. Dini na
siasa vinafanya sehemu muhimu ya maisha ya mwanadamu ya kila
siku.
kimeta Jr
Wewe
Unasemaje?
Sehemu
ya Pili