Munishi:
"Jamani Tutenganishe"
Kuna
msemaji mmoja amesema DINI ni chama. Sasa maoni yangu ni kwamba
mtu awe mwanachama wa chama kimoja tu. Yaani kama ni muumini
wa dini basi asiwe mwanachama wa chama cha siasa.
Ili wanasiasa watafute watu wasio na dini wawe wanachama wao.
Wakiunda serikali waseme haina dini. Hakuna atakayewapinga
kwa hilo. Kwa sasa hawawezi kusema serikali haina dini, maana
waliounda serikali ni watu na dini zao. Na hawajawahi kuzikana
dini zao. Kwa nini serikali inawasaidia kukana kwa niaba yao?
Wewe
Unasemaje?

Pope
asema "Hapana"
waliounda
serikali wana dini zao binafsi lakini unaposema kuwa serikali
ina dini ni kuwa labda imo chini ya dini fulani labda uislamu
kama Misri au Ilivyokuwa Afghanstan au ilivyo Vatican lakini
hii ya kwetu ina WAUMINI WA DINI TU ILA SERIKALI HAINA DINI
WAL HAIFUATI DINI YEYOTE.....
Wewe
Unasemaje?

Munishi
asema "Hapana"
Sina
maana hiyo ila serikali haiwezi kusema haina DINI Labda waseme
serikali ina dini zote za waliounda serikali hapo nisingekuwa
na utata.
Wewe
Unasemaje?

Pope
afurahia ushindi
BASI
INAWEZEKANA TATIZO HAOPA NI LUGHA NA SIO UELEWA . TEH TEH
TEH !!!!!!!! KWA KUWA TOFAUTI YA UTAWALA WA DINI NA SIASA
NI KWAMBA KUNA DINI NYINGI TOFAUTI ZENYE VIONGOZI TOFAUTI
KATIKA NCHI MOJA (Mfano: kadinali, padri na askofu na wakatoliki
wake, sheik na kadhi na waislamu wao, wabudha wahindu wapagani,
walokole nk) NA KUNA SERIKALI MOJA ISIYO NA DINI YENYE KIONGOZI
MMOJA SIJUI UNANIELEWA HAPO?
Sasa linapokuja suala la kiutawala Serikali inatawala na baadae
kuwaruhusu watu kila mtu kuwa na dini yake na hili ni kwa
nchi zisizo na serikali ya dini lakini kama hakutakuwa na
na mtawala mmoja hapo nani atamsikiliza mwenzie?
Wewe
Unasemaje?

Siasa
inanyanyasa DINI: Munishi
Wakisema
serikali ina dini zote, na kiutendaji iwe hivyo. Siyo watu
wa dini kuonekana duni mbele ya serikali. Nadhani waliosema
serikali haina dini lengo lao lilikuwa kuwadhalilisha wenye
dini ili maamuzi ya serikali yasipingwe na watu wa dini.
Wakibadili lugha kama unavyosema, basi dini itajihusisha moja
kwa moja na mambo ya kisiasa. Jambo ambalo serikali nyingi
hazitaki.
Wewe
Unasemaje?

Hapa
kwetu haiwezekani: POPE
Ndugu
munishi ni lazima ujue kuwa Sisa nayo ni mfumo wa Maisha wa
Kiutawala tofauti na Dini you talk about Faith na sehemu ambazo
zinatawaliwa na serikali ya dini labda sehemu kubwa uwe ni
dini tawala lakini kama hapa kwetu kwenye dini kubwa mbili
ya ukristu na uislamu hapatawaliki asikudanganye mtu.
Wewe
Unasemaje?
Munishi
asema Inawezekana
Ndio
maana nilisema kuwa siasa haiwezi bila dini, lakini dini inaweza
bila siasa.
Wakishindwa kuifanya siasa na dini zitawale pamoja na hapa
nina maana maamuzi makubwa yafanywe na dini, basi waachie
ngazi dini zitawale. Zinaweza kufanya hivyo bila siasa.
Kama
yote hayo yatawashinda, basi tusidanganyane. Tutenganishe.
Na kutenganisha ni rahisi. Waumini wa dini wakome kuwa wanachama
wa siasa, na wanasiasa watafute wale wasio na dini wawe wanachama
wao. Halafu tuone kazi hapo.
Mimi mwenyewe siyo mwanachama wa chama chochote cha siasa
na sitarajii kuwa hivyo. Lakini hii hainiondolei haki yangu
ya kuiongoza jamii. kwa sababu siasa imejitwika jukumu hilo
ikashindwa, ituachie wenyewe kwani jukumu la kumwongoza mwanadamu
tangu mwanzo lilikuwa la Mungu akiwatumia watumishi wake aliowateua.
Katika hilo mimi ni mteule wa Mungu kwa Tanzania. Pope unaonekana
ni msomaji mzuri wa BIBLIA. Basi wewe siyo mgeni wa haya niyasemayo.
Waambie akina Kimeta Jr. haya watafurahi kusikia.
Wewe
Unasemaje?

Ndani
ya DINI iko siasa- Al Melech
Ndani ya dini
iko siasa, Vatican iko siasa, Anglican iko siasa. Wale ambao
wanataka kuongoza kidini huwa wana campaign ili wachaguliwe.
Hata pope alipigiwa kura, na hao hutumia siasa chafu.
Wewe
Unasemaje?

Eriksen
Aungana na Al Melech
Al Melech nakusikia
walonga. Siasa chafu ndio siasa gani? Tufafanulie kidogo hapo.
Wewe
Unasemaje?

Pope
amuona mwokozi - Al Melech
Haya
Al Melech na mimi pia nilipigiwa kura ?!!!. Ohooo kumbe Pope
John Paul nikidhani ni mimi Pope Pius haya ni siasa gani chafu
hizo ndugu yangu maana mhh umenigusa pahala yakhe......