Free Web Hosting by Netfirms
Web Hosting by Netfirms | Free Domain Names by Netfirms


Ukurasa wa mbele
Gazeti la injili
Nyimbo za Munishi
Soma barua Yahoo
Soma barua Hotmail
Tuma SMS duniani
Sema nami
Sikiliza waongo
Twende kanisani

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Gazeti INJILI http://munishi.netfirms.com
E-mail: munishifaustin@yahoo.com
Or fmunishi@hotmail.com

Siasa na Dini Zitenganishwe?
Ni kweli Serikali hazina dini?
3


Mavuto apiga msumari kwa karibu
Bwana Al merech nashukuru kwa mchango lakini katika jumuisho ungesema kuwa hivi vitu huwezi kuvitenganisha ila ni matapeli wachache wanajitahidi kutudanganya kwani kama dini ni waumini na siasa ni watu ina maana watu haohao ndio wanachama wa siasa kama sio wanasiasa au siyo?.
Wewe Unasemaje?

Pope afurahia wokovu

INAWEZEKANA KWA UELEWA WANGU MDOGO NIMEELEWA VIBAYA , KWANI MADA NI KWAMBA KIONGOZI WA DINI AU WA SIASA NDIO  AWE UPANDE MMOJA  TU YAANI SIASA PEKEE AU DINI PEKEE  AU WANANCHI KWA UJUMLA KAMA NI WANANCHI SI RAHISI MAANA NI KAMA ALIVYO SEMA aL MELECH HAKUNA DINI BILA WAUMINI NA HAKUNA SIASA BILA WANASIASA AMBAO NI HAO WAUMINI REGARDNESS NI  WA DINI GANI LAKINI KAMA ISSUE NI VIONGOZI BASI NI RAHISI MNO KUTENGANISHA YAANI KAMA KIONGOZI AWE WA SIASA TUU NA KIHUTUBIA ASIGUSIE MAMBO YA DINI NA KAMA KIONGOZI AWE WA DINI TU AKIHUBIRI ASIGUSIE SIASA HILO LITAWEZEKANA NA TUKIANZIA KWA MUNISHI.
Wewe Unasemaje?

Mavuto Amkwamisha POPE
Kiongozi mkweli wa Dini ni lazima awe mkali kwa wala rushwa,wakwepa kodi,chaguzi za uongo na hata uongo wa wanasiasa hasa kwa jinsi nchi yetu ilivyo askofu au sheikh akithubutu kukemea hayo basi tunamwambia anajihusiha na siasa sasa mimi huwa najiuliza kuwa nini maana ya siasa!
Wewe Unasemaje?

Mtu Kwao Akataa kutenganisha
Nini hasa maana ya maneno "DINI" na "Siasa".Tukijua tofauti na mipaka yake, basi tutakuwa na nafasi nzuri ya kuipambanua hoja ya mjadala.

Wakati wa siasa za ujamaa zilipokuwa zimepamba moto, mwalimu wangu wa siasa, kwa mfano, alinifundisha kuwa "siasa ya Ujamaa" ni IMANI. Na dini pia tunaambiwa ni imani. Sasa vitu hivi viwili vilivyo na muelekeo mmoja utavienganishaje? Sijui kama kuna tafsiri nzuri, lakini naona ni vigumu kuvitenganisha IMANI mbili hizi kwa mtu mwenye IMANI.
Kinachowezekana ni kubabaisha na kuwazubaisha watu  kwa lengo la kusanifisha matakwa yake.

Na sisi wafuasi tena tunasema "Mfuate Kafiri, upate mradi wako"

Wewe Unasemaje?

Munishi bado yumo
Kama uko mzima Mtu Kwao, Machale yamenicheza. Nisubiri hapo naja sasa hivi. Imani mbili atakuwaje nazo mtu mmoja? Wenye imani ya dini wabaki nayo. Na wenye imani ya siasa wabakie kwao. Tutenganishe bwana. Maji na mafuta lini yakachanganyika kabisa?
Wewe Unasemaje?

Mavuto ajaribu kupotosha
Munishi mtu kwao kakusubiri sana hukutokea sasa ulivyosema hiyo mara moja utarudi ulikuwa unamaanisha nini??
Wewe Unasemaje?

Munishi amfuata Mavuto porini.
Mavuto.
Kwa nini unapenda kumuonea Mtu Kwao? Sisi na Mtu Kwao tunaelewana sana.

Mavuto Azidi Kwenda Porini.
Munishi mimi sio kwamba namuonea Mtukwao ila naona Mzee unataka kumchokoza ndugu yangu Mtukwao aanze vitu vyake vibaya hivyo bwana,sasa Mtu kwao naona kamkazania Pengo ina maana ZNZ haionewi tena na Bara? jee na Uislamu nao kashaacha kuutetea!
Wewe Unasemaje?

Mtu Kwao Porini Kwa Lengo
Bwana Mavuto nadhani unataka kuipotosha mada. Unataka tuanze mjadala ndani ya mjadala. Na mwenzangu kwa bahati mbaya ni "mwepesi".  Nikikupa kijiba kidogo, maradhi ya moyo tayari, hata hujapewa siri ya sufuri!
Funika kombe mwanaharamu apite
Wewe Unasemaje?

Munishi awatoa wote Porini
Jamani Dini na siasa Zitenganishwe? Mi9mi naona zitenganishwe. Mambo mengine baadaye.Kwa sasa Je DINI na siasa zitenganishwe kabisa.
Wewe Unasemaje?

Mtu Kwao arudi kwenye Hoja
Kusema dini na siasa zitenganishwa ni rahisi na jambo zuro kinadharia. Sasa swali, tuzitenganishe vipi?
Nashindwa kuamini kama hali hiyo itatokea,kwa sababu imani iko juu kwa kila kitu.
Nikiamini mimi kuwa 2+2=5, basi itakuwa unakazi kubwa kunieleza tofoati. Nitahoji kwa nini iwe nne na isiwe tano? Si kuamua tu kuanzia sasa 2+2=5. Kuna uhalali gani kuwa lazima iwe nne. Huu ni mfano wa imani kiasi cha kunipa mashaka kuwa Dini na Siasa ni IMANI kuweza kutenganishwa.

Siasa ni mfumo wa maisha na mawazo ya kuendesha kitu fulani.

Dini nyengine ni mfumo wa maisha, desturi  sheria na mila.
Bwana Munishi unaweza kujua hili ni tui na haya ni Maziwa, lakini ukifanya kosa kuyachanganya, basi asili ya vyote umepoteza na huwezi kujua au kutenganua tena. Kwa ufupi huwezi tena kupata maziwa yako au tui lako. Na sasa hiyo ni hatari. lazima tuangalie mbele. Hatari mti na macho!

Wewe Unasemaje?

Mavuto amsifu Mtu Kwao
Mtu kwao unazidi kuimprove ndugu yangu manake hako kahoja kako nimekasoma na kuona kana mantiki kwelikweli wakati unaandika ulikuwa na Marandu,Pope au mzee Munishi???
Wewe Unasemaje?

Munishi Atibua Maji
Siasa hazikuwahi kuchanganywa na dini kama alivyosema mmoja wetu hapa. Lakini siasa inatumia dini kutawala.

Utaniuliza sasa tunatenganisha nini kama hazikuwahi kuchanganywa?

Tunatenganganisha kudanganyana. Na hapa mdanganyifu ni siasa. Inawakuta watu wakiwa na dini zao, inawapa kadi za chama cha kisiasa, halafu sijui wanafanyaje vile? Wanaiba kura na kusema wameshinda uchaguzi. Tatizo linaanzia hapo. Baada ya kuunda serikali, wanasema kuwa hiyo serikali haina dini. Mambo yanakuwa mabaya zaidi wakati serikali hiyo inapoua watu mfano kule Zanzibar. Hawataki watu au viongozi wa kidini wawakemee. Wakifanya hivyo wanaitwa wachanganyaji wa siasa na dini.

Hii ni kuonyesha kuwa wanasiasa hawataki siasa ichanganywe na dini. Lakini hapa pia nashangaa kuona kuwa wanasiasa hao hao hawataki siasa na dini zitenganishwe.

Hawataki zichanganywe, wala kutenganishwa. watuambie wanataka zifanyweje?

Huwezi kutenganisha vitu ambavyo havijachanganywa, na pia huwezi kuchanganya vitu ambavyo havijatenganishwa. Nionavyo mimi ni kwamba siasa inatumia dini kwa ujanja. Wakati umefika wa dini kukataa kutumiwa kwa hila za kisiasa.

Sasa iite utakavyo kutenganisha, au kuachanisha. kusambaratisha au kutegemeza dini pekee. Au unaweza kusema DINI yaishtukia siasa. Pengine iwe hivi: SIASA NA DINI KILA MTU LWAKE. Unaonaje hii: Waumini wa dini wachoma moto kadi zao za chama cha kisiasa. Wasema wamechoka kutumiwa kwa manufaa ya wanasiasa na siyo Mungu. Vyovyote utakavyoiita, tayari kuna haja ya kujadili kwa undani sana masuala ya dini na siasa katika jamii yetu. Dini na waumini wake wanajisikia kunyimwa haki zao za msingi na wanasiasa ambao kimsingi hawawezi bila dini. Mungu ni mkuu kuliko wanasiasa, lakini dini hupewa kibali cha kumwabudu Mungu na wanasiasa. Isitoshe wao ndio wanaoweka jinsi na namna ya kuabudu. Kuna mmoja anayemdanganya mwingine hapa. Siasa ndiyo mdanganyifu hapa. Sasa basi. Imetosha. Tunataka kumwabudu Mungu kama alivyosema na siyo kama wanasiasa wanavyotutaka tuabudu.

Kwa kuwa zote ni imani, kila moja ina Mungu wake. Siasa kamungu kake ni wanadamu, wakati dini Mungu wake ni Mungu Mkuu. Basi tutengane kabisa. Na hii italazimu mmoja aachie ngazi kabisa. Siasa ndiyo ikome duniani. Na dini ichukue hatamu zote kuiongoza dunia.
Wewe Unasemaje?

 
| http://munishi.netfirms.com |
 
<<Back  |  Home |  Gazeti La Injili | Injili2 | Nyimbo Za Munishi | Next >>